Aina za Nomino

Nomino ni majina ya watu, vitu, mahali, au wazo. Kuna aina nyingi za nomino k.v.

  • Nomino za Kawaida
  • Nomino za Pekee
  • Nomino za Wingi
  • Nomino za Dhahania
  • Nomino za Vitenzi-Jina
  • Nomino za Makundi

1) Nomino za Kawaida

Nomino za pekee ni maneno yanayorejelea vitu vya kawaida kama vile watu, nyumba, mahali, mimmea na vitu. Nomino za kawaida hazitumii herufi kubwa katikati ya sentensi kama nomino za pekee.

Mifano ya Nomino za Kawaida: Mkahawa, nyumba, mti, mwalimu, sahani, chupa, meli, mtoto, mwanafunzi, mtu, mji, mnyama, mbwa, ndege

2) Nomino za Pekee

Nomino za pekee ni majina spesheli yanayotumiwa kutambua nomino za kawaida kwa ubinafsi. Maneno yanayotaja majina mahususi ya watu, mahali, au vitu ambavyo vina sifa ya kipekee. Nomino za pekee hutumia herufi kubwa katikati ya sentensi.

Mifano ya nomino za pekee: Kemboi, Kisumu, Tom, Anna, Afrika, Ulaya, Nairobi, Kamau, Mlima Kenya, Tanzania, n.k.

3) Nomino za Wingi

Nomino za wingi ni nomino zinazorejelea vitu vinavyopatikana katika uwingi. Ni nomino ya vitu visivyohesabika.

Kwa mfano: Maji, mchanga, supu, chumvi, sukari, damu, wino, maziwa, mate, wali, mvua, unga, samli.

4) Nomino za Dhahania

Nomino za dhahania ni majina ya vitu visivyoweza kuonekana au kushikika kwa mkono. Ni maneno ya vitu vya kufikirika tu.

Mifano: Usingizi, shibe, furaha, huzuni, hekima, ubinafsi, uchoyo, maumivu, upendo, ukorofi, upole, ujinga, werevu, wema, kiu, elimu, ugonjwa.

5) Nomino za Makundi

Nomino za makundi ni nomino zinazohusika na vitu vinavyopatikana kwa makundi. Pia huitwa nomino za jamii.

Mifano ya nomino za makundi:

  • Thureya ya nyota
  • Halaiki ya watu
  • Umati wa watu
  • Mlolongo ya magari
  • Fungu la maembe
  • Baraza la wazee
  • Shada la maua
  • Chane ya ndizi
  • Funda la maji
  • Shehena ya mizigo
  • Biwi la takataka
  • Msafara wa magari

6) Nomino za vitenzi-jina

Nomino za vitenzi-jina ni nomino zinazoundwa kutokana na vitenzi kwa kuongeza kiambishi “KU” mwanzoni mwa mzizi wa kitenzi.

Mifano: Kulea, kusoma, kulia, kucheka, kulima, kuandika, kutibu, kutesa, kuona, n.k.

Sentensi: Kucheka kwangu kumewaudhi wanaharakati wa mazingira.

(Visited 23 times, 1 visits today)

KCSEPDF.CO.KE

kcsepdf.co.ke is an online learning platform where tutors and students can access notes, revision questions, educative articles, stories, e-books, and more learning materials.

Leave a Reply

Kiswahili Notes and Past Papers

Mambo ya kuzingatia unapoandika insha

Kuna baadhi ya mambo au masharti ya kuzingatia ili uandike insha bora. Hati nzuri inayosomeka kwa urahisi Mpangilio mzuri wa hoja – kila aya lazima iwe na hoja maalum iliyoelezwa kwa upana na ufasaha. Urefu wa kutosha wa insha – sana sana ukurusa moja na nusu had kurasa mbili. Lugha sanifu isiyokuwa na makossa ya […]

Read More
Example of KCPE Insha
Kiswahili Notes and Past Papers

How to Pass in KCPE Insha Paper

Aina za Insha Katika shule ya msingi, wanafunzi hufunzwa aina nyingi za insha: Insha za methali Insha za mjadala Insha za Mdokezo Insha za Mada Insha ya mahojiano Insha za Mjadala Katika insha ya mjadala, mwanafunzi anatakiwa kutoa hoja za kuunga mkono au kupinga mada fulani. Kwa mfano: Andika insha ya mjadala kuhusu mada: Serikali […]

Read More
Kiswahili Notes and Past Papers Revision Notes and Questions

Kiswahili KCSE Past Papers

Hello, you can download free KCSE question papers for Kiswahili here. Access past KCSE question papers and free KCSE revision papers; free download PDF. KCSE-2011-KISWAHILI-PAPER-1 KCSE 2011-KISWAHILI-PAPER-2 KCSE-2011-KISWAHILI-PAPER-3 KCSE-2012-KISWAHILI-P1 KCSE-2012-KISWAHILI-P2 KCSE-2012-KISWAHILI-P3 kiswahili-paper-1-form-3-term-1-exam-2018 kiswahili-paper-1-term-2-exam-2018 kiswahili-paper-2-form-3-term-1-exam-2018 kiswahili-paper-2-term-2-exam-2018 kiswahili-paper-3-term-2-exam-2018

Read More